readenglishbook.com » Religion » Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗

Book online «Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗». Author Susan Davis



1 ... 6 7 8 9 10 11 12 13 14 ... 17
Go to page:
hawajeiwahi kukitayarisha. Kuna mabadiliko mengi ambayo hivi karibuni yatatendeka duniani. Nataka mwamini ukweli huu.

Wana, saa yangu ya kurudi imefika. Naona kuwa wengi hawajajitayarisha. Wengi wanamini wa tayari ila siyo hivyo. Wengi bado wanacheza na dunia. Hii haiwezekani. Wanangu, vunjeni uhusiano na dunia. Dunia hii ni meli inayozama na itazama nanyi.

Wanangu, sifurahiswi na jinsi mnavyo fukuza vitu vya dunia badala ya kunifuata. Mwatafuta majibu kutoka kwa dunia. Haiwezekani wanangu.

Mwatazama tumaini lilo bure… Ahadi za bure … ukweli ulio bure. Majuta ikiwa mtaendelea kuifuata hii njia isiyo na matumaini yo yote. Mbona mnaendelea kuamini kuwa dunia itawapa majibu hali mimi ndiye ukweli.

1 Yohana 2:15. Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

Wana, sikizeni kwa makini, wakati wenu unakwisha. Mna muda mdogo sana wa kujitayarisha. Wakati wa kujitayarisha ni huu. Ikiwa mnataka kuja nami, ni sharti mzingatie kurudi kwangu. Adui wangu anajitayaisha kutenda mambo yake hivi karibuni. Mipango yake itaharibiwa tu na kurudi kwangu.

Wanangu, hamuoni kuwa ni sharti muwe macho na tayari kwa matukio ambayo ya karibu kutendeka? Hivi karibuni kila mtu ataathiriwa na mabadiliko yajayo duniani. Aidha mnakuja nami pahali pa salama au mnabaki ili mpambane na adui wangu na ghadhabu yangu ijayo.  

Siku hii yaja, wanangu. Yaja na hakuna awezaye kuizuia. Mwafaa mjitayarishe maana wakati u karibu. Waja kwa upesi.

Njooni mnijue. Hamna njia nyingine. Msipotenga wakati wakunijua, basi hamtaweza kuja nami mahali pa usalama.

Lazima mjitolee na kuniachia kila kitu kilicho chenu. Nawasubiri wanangu. Nani atakaye nijia kwa kujitolea kikamilifu? Nani atakaye kuja ili anijue, anijue kweli. Hivyo ndivyo ninavyohitaji.

Niliwatengenezea njia. Nimewatengenezea njia. Nimelipa gharama kubwa sana kwa ajili yenu ili muwe huru ili muweze kuwa nami nitakapokuja kumchukua bi arusi wangu. Bi arusi wangu yu tayari nami namjia.

Gharama niliyolipa ilikuwa kubwa sana. Hakuna ye yote ambaye angefanya nilivyofanya. Ni mimi tu ndiye nigeweza kutimiza yale niliyotenda. Ni mimi tu ningeweza kulipa gharama kubwa kiasi hicho – Mungu ambaye alijiweka kua kiwango cha binadamu na kupondwa kwa ajili ya binadamu. Gharama hi haiwezi kuhesabika. Hakuna thamani inayoweza kuwekwa kwa kitendo hiki. Hakuna kiasi cha fedha kinachoweza kulipa gharama iliyolipwa.

Isaya 52:14. Kama vile wengi walivyostajabia uso wake ulikuwa umeharibiwa sana zaidi ya mtu yeyote, na umbo lake zaidi ya wanadamu.

Wana, msiikatae zawadi kama hii. Njooni, nawapa zawadi hii bure. Naomba muichukue zawadi inawangoja muichukue ili muwe huru, huru kuja kwangu na kwenda nami nitakapokuja kuwavuta wanangu ili wapate uhuru.

Hii zawadi ni yenu. Njooni kwangu na mjitolee kwangu. Nipeni yenu yote yanayowahusu. Ninachotaka tu ni ninyi muniachie maisha yenu yote niyatawale. Msipokuja kwangu na kuwa wana wangu, mtakuwa mngali wana wa adui wangu. Hamna lenu. Aidha ninyi ni wangu au ni wa adui wangu. Nichagueni. Nangoja jibu lenu.

Huyu ni BWANA na MWOKOZI, YAHUSHUA, MASIYA MKUU.

 

 

SURA YA 19: JITAYARISHENI

Natuanze (Februari 19, 2012). Wana, nina maneno: Wakati wa kurudi kwangu unakaribia. Mnahitaji kujitayarisha. Nataka niwachukue nimkujiapo bi arusi wangu, mrembo, bali ikiwa hamtakuwa tayari, sitawachukua.

Ni sharti mjitayarishe. Mnionyeshe kuwa mu tayari. Nawataka muwe mkinitazamia. Nataka macho yenu yawe kwangu. Ikiwa haunitazami, basi hauko tayari. Wale wanaonitazamia tu ndio walio tayari.

Waebrania 9:28 kadhalika Kristo naye, akiisha kutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi; atatokea mara ya pili, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu.

Wengine wanasema hawahitaji kunitazamia ili wawe tayari. Huu ni uongo kutoka kwa adui. Ni mjanja na mwingi wa udanganyifu. Anataka kuwaongoza wanangu mbali na kuwatoa kwenye njia nyembamba. Ni lazima muwe tayari kila wakati. Ni sharti mnitazamie na kujitayarisha kwa maana hamjui saa nitakayo rudi. Nitakuja kama mwizi usiku. Je, neno langu halisemi hivyo? Neno langu li wazi kuhusu jambo hili. Wengi watapigwa na bumbuazi. Hawatakuwa tayari kwa maana walikataa kunitazamia na kusimama imara.

Msiwe kwenye kundi hili ambalo linakataa kutii maonyo yangu na yakunitazamia na kuwa tayari. Kundi hili litahuzunika sana na kufadhaika likigundua kuwa wameachwa ili wapambane maafa ya dunia na misukusuko ya binadamu.

Msiwe wanyamavu nawasiotenda lolote kwa ajili ya maonyo mengi niwapayo. Kuweni tayari! Amkeni!

2 Timotheo 4:8. Baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake. 

Wanangu, hata mnaruhusu kazi zenu za huduma ziwafanye msijitayarishe na tukio hili kuu. Makanisa mengi na viongozi wangu wengi wataachwa. Msipatikane mtegoni humu. Muwe macho. Muwe tayari. Mjihadhari.

Usiache nyumba yako invunjwe na mwizi. Usisimame tu kando ukiangalia nyumba yako ikivunjwa na mwizi. Mlinzi asiyejitayarisha atashtuka mwizi akija bila matarajio. Jilindeni. Jitayarisheni kwa maana hamjui saa ile nitakayorudi. Wakati mnapodhani kuwa siji ndipo nitakapo kuja.

Nikishamchukua bi arusi wangu, kanisa langu, sitarudia na hii njia tena. Mlango utafungwa na hakuna binadamu atakaye weza kuufungua.

Luka 13:24-25 Wakati mwenye nyumba atakapo simama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema Ee, Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia Siwajui mtokako.

Kurudi kwangu ni kwa haki na upesi. Sitachelewesha tukio hili kwa ajili ya mtu yeyote au kitu chochote. Laja, hakika laja. Kesho huenda ikawa umechelewa. Hivyo ndivyo kurudi kwangu kulivyo karibu. Msichelewe kwa uamuzi wenu na kujitayarisha kwa kurudi kwangu. Mkingoja sana mtanikosa. Huu si wakati wa kuchelewa na kurandaranda kwa njia za dunia.

Wana, msingojee kufanya uamuzi. Sitalisubiri milele ili kanisa langu vuguvugu liamke. Nawaomba myaweke maanani maneno haya. Sitaendelea kulisubiri kanisa ambalo linakataa kunifuata na kunitafuta. Haiwezekani.

Nitaendelea na mipango yangu na kuwachukua walio tayari. Wanaonitafuta kwa bidii, na kunisubiri kwa matarajio makuu. Hawa ndio nitakaowachukua… wengine wote wataachwa.

Nawaomba msamaha ikiwa maneno yangu ni magumu. Maonyo yangu yamekuwa wazi na bila kusita. Mbona watu hawaamini neno langu? Je, mimi MUNGU sijakuwa hivyo? Mimi sibadiliki.

Waebrania 13:8 Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele.

Jitayarisheni, kwa maana ni tayari kumchukua mpendwa wangu. Ni tayari kumchukua. Ikiwa unataka kuwa mmoja wa bi arusi wangu, basi jitayarishe. Wakati ni huu “sasa”. Jitayarishe.

Muda unakwisha. Tazama na kujitayarisha. Haya ni maneno yangu. Nami hutimiza maneno yangu.

BWANA WENU YAHUSHUA.

 

SURA YA 20: WAKATI WENU U KARIBU KWISHA.

Natuanze (Februari 20, 2012). Ni tayari kukupa maneno: Wana, Ni mimi, BWANA wenu na ni hapa kuwapa muelekeo mpya.

Dunia inakwisha upesi. Wakati waja wa dunia kuipata gadhabu yangu. Saa hii yaja upesi, wana, kwa kasi mno. Kuna wakati kidogo sana umebaki, kila mmoja ataweza kuelewa. Ni hivi karibuni.

Ufunuo 14:10: Yeye naye atakunywa katika mvinyo wa gadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana- Kondoo.

Wana, kaeni chonjo na kuwa macho. Msitupilie mbali maonyo haya muhimu.Tieni bidii kwa kujitayarisha. Kurudi kwangu ku karibu sana. Hakuna wakati wa kupoteza. Amkeni!. Sitawasubiri milele. Siwezi. Ni sharti nimuondoe bi arusi wangu natuondoke. Yu tayari. Amejitayarisha. Nawataka ninyi muwe tayari pia. Wanangu, njooni kwangu kwa unyenyekevu. Hii ndio saa yangu ya kurudi.

Msingonjee milele. Hamna “milele”. Wakati wenu u karibu kwisha. Najua haya yanawajia kwa mshangao nakutoamini, ila ukweli ni kuwa wakati umefika wangu mimi kumuondoa bi arusi. Yu tayari, ni tayari, na dunia imenipa kisogo.

Hivi karibuni, bi arusi wangu aningojeaye hataningojea tena. Sitamruhusu abaki nyuma na kukumbana na yale yajayo kwa walio duniani ambao wamenigeuka. Amejitayarisha na wakati wake wa kuondolewa na kupelekwa mahali pa usalama umefika.

Ufunuo 19:7. Natufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

Hili litakuwa tukio kuu lisilolinganishwa na linguine lote katika historia ya binadamu.  

Wana, jitayarisheni ili mje nami. Tukutane hewani. Nataka niwachukue mwende nami pahali pa usalama. Hivi karibuni itatendeka.

Msidanganywe na dunia. Wengi wanakwamilia kwa dunia wakidhani kuwa itawapa majibu. Dunia ina simanzi na hofu. Msihangaishwe na maonyo haya. Yakubali maana ni ukweli.

Kiangalieni kitabu changu. Kisomeni. Fungueni kurasa zake. Acheni ukweli wangu ufunuliwe mbele yenu, ukweli wangu.

Nitafuteni mimi. Fuateni Roho wangu. Acheni Roho wangu awaonyeshe ukweli. Mruhusuni aje maishani mwenu na awape kuelewa kupya kwa neno langu. Binadamu hawawezi kuwaonyesha ukweli. Roho wangu tu.

1 Wakorintho 2:11-14. Maana ni nani katika binadamu ajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. Lakini sisi hatukupokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.

Wana, saa hii inakaribia. Niacheni nizitendee kazi roho zenu. Niacheni niwaoshe kwa damu yangu ya ukombozi. Niacheni nizifunike dhambi zenu na damu yangu iliyolipa fidia msalabani. Huo msalaba wa aibu ambako nilivuja damu hadi kufa kwa ajili ya dhambi zenu. Nilifanya haya yote kwa ajili yenu wanangu. Ninyi wote..nilivuja damu kwa ajili yenu….wale wote watakao ikubali zawadi hii ya bure.

Wafilipi 2:8. Tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

Naam, ulikuwa upendo wangu na matakwa yangu kuwaokoa wanadamu kutoka kwa makosa kwa ajili ya laana za dunia hii. Hii zawadi ni yenu pia ikiwa mtakubali kuichagua na kuichukua na kupata msamaha wa njia zenu mbovu.

Ni sharti mu ihitaji. Ni sharti mje kwangu kwa kujitolea kikamilifu. Nataka kuwaona mkiachana na upendo wa dunia na mambo yote yanayohusu dunia. Hamwezi kuwa kwenye ufalme wangu ikiwa mngali na mapenzi kwa dunia.

Kwa hivyo mna uchaguzi wa kufanya! Njia zangu ama mnachagua kwenda kwa njia zenu wenyewe pamoja na adui wangu? Hakuna kuwa katikati. Ni upande mmoja au mwingine. Hiari yenu au hiari yangu. Lazima mchague.

Ikiwa mtachagua mapenzi na hiari yangu, ni sharti mje kwa unyenyekevu na kutubu dhambi zenu. Nitawafunika kwa damu yangu na kutoa dhambi zenu zote. Kumbukumbu zote zitaharibiwa na maisha yenu yatakuwa mapya.

Waebrania 13:12. Kwa ajili hii, Yesu naye, ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe aliteswa nje ya lango.

Haya ndiyo yawangojayo ikiwa mtakuja kwangu kwa kunyenyekea na kutubu dhambi zenu. Huu ndio wakati wa uamuzi huu. Msingojee. Wakati wa kurudi kwangu umewadia. Hakuna binadamu awezaye kuisimamisha saa hii.

Mwafaa mjitayarishe. Jitayarisheni. Nasubiri jibu lenu.

Huyu ni wenu Mstahamilivu, Mungu mpendwa, YAHUSHUA.

 

SURA YA 21: MBALI NA MAPENZI YANGU, MWANIPINGA
1 ... 6 7 8 9 10 11 12 13 14 ... 17
Go to page:

Free e-book «Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗» - read online now

Comments (0)

There are no comments yet. You can be the first!
Add a comment