readenglishbook.com » Religion » Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗

Book online «Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗». Author Susan Davis



1 ... 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17
Go to page:
kuona katika pembe zote za moyo na dhambi iliyofichwa humo isiyoonekana na mtu mwingine yeyote.

Jeremiah 17:9. Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nami awezaye kuujua?

Niacheni niisafishe miyo yenu, iwe safi. Niacheni nizitakase nafsi zenu. Niacheni niwaweke tayari kusimama mbele yangu. Ni mimi tu niwezaye kutenda haya.

Ni mimi tu niwezaye kuwakamilisha kupitia damu yangu niliyotoa kugharamia dhambi zenu. Natamani kuwapa damu hii ili iwatakate na kuwafanya kuwa wasatafi.

Matendo ya Mitume 22:16. Basi sasa, unakawilia nani? Simama, ubatizwe, ukaoshe dhambi zako ukiliita jina lake.

 Wana, wanangu, nawasuburi mje kwangu kwa toba, toba ya moyoni. Njooni kwa mwanga wangu: pokeeni wokovu wangu, wokovu nilioununua kwa damu yangu. Ni mimi tu pekee niwezaye kuwatendea haya. Niachieni maisha yenu yote. Msiogope. Dunia inaporomoka. Haina majibu yote, ukweli wowote haina. Siyo ya kutegemewa. Miye ndiye mwamba. Ni mimi tu niwezaye kuaminiwa na maisha yenu. Nipeni maisha yenu. Hata msipoelewa maana yake, niachieni maisha yenu.

Niachieni maisha yenu nami nitayachukua na kuwajali. Nitawafanya tunu yangu na kuwajaza na upendo wangu, Roho wangu, na amani yangu. Inayopita vyote. Amani msioyoweza kuelewa. Amani ya mungu. Itokayo kwa Mungu, Mungu Mtakatifu. Mnastahili amani kama hii ya milele. Ni mimi pekee ninayeweza kuwapa amani hii.

Hii ndio saa ya kunena imani yenu kwangu. Mnichague. Msiponichagua, mtakuwa mumemchagua adui wangu. Kuna mawili tu -- mawili tu. Aidha u nami, au unanipinga. Hakuna nafasi ya tatu. Msidanganywe. Hata mkiwa ukingoni, ninyi si wangu. Nataka mjitolee kikamilifu.

Njooni kwangu kwa toba iliyo kamilifu, na nitaziondoa dhambi zenu, jinsi mashariki ilivyo mbali na magharibi. Sitaziangalia tena. Nitawafanya wasafi. Tutashiriki katika uhusiano wa karibu na mtanijua na kunifahamu vyema. Natamani tujuane hivi.

Zaburi 103:12. Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi, ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi.

Kwa hivyo njooni mpate kunijua. Ninastahili kuwa na uhusiano nanyi. Nitawaleta pahali pa amani na uelewano. Roho wangu atawaongoza na kuyafungua macho yenu ili mwone ukweli; ukweli unaoyakoa maisha yenu. Atawaonyesha wakati mlio ndani. Atawaonyesha ukweli kwa njia msioweza kuelewa, na mtaokolewa na kuwa na pahali katika ufalme wangu. Haya ndio matamanio yangu. Njooni muweze kumjua huyu Mungu wenu. Tetembee pamaja mkono kwa mkono. Nitawapeleka nje ya dunia hii. Wakati unakwisha. Nichagueni.

Ni mimi BWANA wenu na MWOKOZI wenu MKUU MASIYA Mfalme Mkarimu YAHUSHUA.

 

SURA YA 24: ACHENI KUPIGANA WENYEWE KWA WENYEWE

 Natuanze. Wanangu, leo nina maneno ya kuwapa. Yote si muonavyo. Mambo yatabadilika hivi karibuni. Wanangu, kuna kuwa giza. Kila kitu ni giza. Maisha myajuavyo yanabadilika sana. Hivi karibuni hakutakuwa na kurudi nyuma.

Hili ndili onyo langu. Nawapa maonyo makali ila ni wachache tu wanao yatilia maanami. Ni wachache sana wanaonisikiza. Mbona wanangu hawasikizi? Wako kwenye dunia yao-sio dunia yangu, sio mawazo yangu, sio maonyo yangu. Yasikitisha mno, wanangu. Siwapi maonyo kwa manufaa yangu bali ni kwa manufaa yenu. Ninafahamu yatakayo tendeka na niwataka mfahamu vile vile.

Mathayo Mtakatifu 6:24. Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.

Wana, sitaki muwe gizani. Nawatakeni mjue ukweli. Nawataka muwe kwenye ukweli wa yale ambayo ya karibu kutukia. Nawaomba mwamke! Nuseni uovu…u kwenye hisia zenu. Kila kiti ni kiovu. Hakuna atakaye utakatifu. Kila mtu amepotea.

Isaya 53:6. Sisi sote kama kondoo tumepotea, kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe. Na BWANA ameweka juu yake maovu yetu sisi sote.

Bi arusi wangu pekee ndiye mwaminifu. Yeye pekee ananitazamia. Pekee ndiye anitakaye nirudi. Anitafuta kwa kila jambo na kwa kila pembe. Huyu ndiye bi arusi wangu, kanisa langu, kanisa langu la kweli.

Wana, acheni kuzozana. Mnaangamizana Acheni kubishana kuhusu maneno yangu. Huu sio wakati wa kuwa na hasira kwa ndugu au dada yako. Adui ameingia kati yenu na kuwadanganya. Anataka kuwaweka kiwango sawa naye. Naomba mwache ubishi usio na maana kati yenu na mpendane.

Yohana 13:34 Amri mpya nawapa, mpendane kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.

Hii siyo njia. Siyo njia yangu. Tubuni wanangu. Kisha muwaende wenzenu na kusuluhisha mambo. Sameheaneni. Muda unaisha. Msiache mambo madogo madogo yaliyo kati yenu. Yawaweke mbali na wokovu wangu wa milele.

Mathayo 6:14-15. Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.

Ninataka kuwaweka huru kutoka kwa dhambi hii. Hakuna dhambi duniani ambayo ni ya thamani kuu kukufanya uupoteze wokovu wako wa milele. Tafadhali likumbukeni jambo hili. Wana, upendo wangu ni mkuu, lakini siwezi kutozingatia dhambi. Kwa hivyo, tubuni leo na msameheane. Likimbilieni jambo hili msiache cho chote kibakie. Wasameheni wote, ndipo baba yenu aliye mbinguni, awasamehe. Hili ni jambo rahisi sana la kusamehe na kuacha machungu yaliyo mioyoni mwenu.

Niacheni niwaponye. Ziwekeni simanzi zenu mabegani mwangu na muniache niwaletee uponyaji. Ni mimi tu niwezaye kuyatenda haya. Njooni kwangu nami nitaichukua mizigo yenu. Nitafanya hiyo kwa hiari yangu.

Niacheni niyajenge maisha yenu na kuondoa uchungu wenu. Nileteeni uchungu wenu. Wasamehe walowakosea na mje kwangu kupata afueni kutoka kwa mizigo yenu. Ningependa kuwapa mioyo mikamilifu.

Lisomeni neno langu. Mimi ni Mungu wa urejesho. Niacheni niwarejeshe kwa ukamilifu na raha. Mimi ndimi nirejeshaye na kuweka kuwa kamilifu. Hakuna mwingine. Niacheni niwaonyeshe mapenzi ya dhati.

Yoeli 2:25 Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa. Nilituma kati yenu.

Ndiyo, hii saa inawadia ya kurudi kwangu. Niacheni niwasafishe na kuwarudishia uzima mpya ndani yangu. Niacheni niwatayarishe kwa kurudi kwangu. Nitayari. Mimi ndimi tumaini lenu, tumaini la pekee. Njooni kwangu. Huu ndio wakati. Msingojee sana. Mimi tu ndiye ninayestahili. Mwana Kondoo ndiye anayestahili. Njooni mikononi mwangu haraka.

Huyu ni BWANA wenu, YAHUSHUA.

 

SURA YA 25: SITAWACHUKUA IKIWA MNGALI MNA DHAMBI AMBAYO HUMJATUBU

Tuanze. Ni tayari kukupa maneno mengine mengi. wana, saa ya kurudi kwangu inakaribia. Itakuja kwa wakati uliopangwa.

Wengi wanadhani kuwa sitawahi kuja. Wengi wanadhani sitakuja hivi karibuni. Wanadhani kungali na miaka mingi sana inayosalia ndipo nije. Wanangu, naja hivi karibuni. Kurudi kwangu ku karibu. Hata mlangoni. Wengi watapatwa bila kutarajia. Wengi watakuwa wamelala, wamelala kiroho.

1 Wathesalonike 5:6. Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

Hivi karibuni, wakati utafika. Wale wanaonitazamia na kuningojea watakuwa tayari. Wale wasio macho wataachwa ili wakabiliane na yajayo. Wakati u karibu sana.

Wana, mnafaa kuwa tayari. Msipatikane bila kujua. Sitaki kumuacha yeyote nyuma, ila ina huzunisha sana maana wengi wataachwa. Ni wakati wa kuhuzunisha sana. Nataka muamke. Mkaamini kuwa wakati huu kweli waja. Naja na hata ni mlangoni. Hivi karibuni, hakuna atakayeshangazwa na yajayo kwa maana ukweli utajulikana wakati watagundua kuwa yote ambayo niliwaambia ni ya kweli. Dunia itatambua kuwa mabadiliko makuu yametendeka. Hivi karibuni, dunia haitakuwa vile imekuwa. Itabadilika.

Wanangu, msikize kwa makini. Sitachukua yeyote ambaye angali na dhambi ambayo hajatubu. Siwezi kuwachukua. Haiwezakani. Kwa hivyo, njooni mbele zangu na mtubu.

Luka Mtakatifu 13:5 Nawaambia, sivyo lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.

Njooni msuluhishe mambo kati yenu nami. Natamani kuwaleta ufalmeni mwangu. Nataka kuwaokoa kutokana na maafa yajayo.  

Siwezi kuwachukua wasio wangu. Ikiwa hujaja mbele zangu na kunipa maisha yako basi wewe si wangu. Hili ni jambo la muhimu sana wanangu. Munahitaji kunipa maisha yenu. Niyaweke chini ya miguu yangu bila kusita. Huu ndio wakati wenu wakuja kwangu kwa unyenyekevu na toba. Nileteeni mahangaiko yenu yote. Nayataka maisha yenu. Nitayabadilisha maisha yenu ya mahangaiko na maisha ya upendo, furaha na ukamilifu. Karibuni, hivi karibuni, naja na ningewapenda muwe tayari. Wakati huu umewadia. Niruhusuni niwape ukamilifu wamaisha. Upendo wangu utazifunika dhambi zenu zote. Njooni kwangu. Nawangojea kwa mikono wazi. Mikono inayotamani kuwakumbatia na kuwapenda.

Mtakatifu Luka 5:31 Yesu akajibu akawambia, Wenya afya hawana haja na tabibu, isipokuwa walio hawawezi.

Msichelewe. Huu ni wakati muhimu sana. Sitachelewa kumtoa bi arusi wangu. Ni tayari kumpeleka nyumbani kwa majumba niliyo mtengenezea. Hapa ndipo atakapoenda ili awe salama. Kwa hivyo wanangu, jitayarisheni, maana kurudi kwangu ku karibu. Nazungumza nanyi kama BABA awapendaye na kuwajali. Nataka kuwaokoa niwaondoe kwenye dunia ambayo hivi karibuni itakua kama kichaa. Niacheni niwaonyeshe mlango wa kuwapeleka mahali salama. Huo mlango utafunguka hivi karibuni. Kisha utafunga. Kwa hivyo jitayarisheni. Ni tayari kuwapokea. Huyu ni BWANA MUNGU wenu kutoka mbinguni YAHUSHUA.

 

 

SURA YA 26: NITAZAMENI

Luka Mtakatifu 13:24-25. Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawambia ya kwamba wengi watataka kuingia wasiweze. Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako.

Natuanze tena. Wana, huyu ni BWANA wenu anayezungumza nanyi. Nawataka mnitazame mimi. Huu siyo wakati wa kukimbia hapa na pale na kutazama dunia. Huu ni wakati wa ustadi. Huu ni wakati wa kunitazamia mimi na kuwa macho kuhusu kurudi kwangu. Kila siku, wakati unakaribia.

Msiyapuuze maonyo yangu. Maonyo haya yanatokea pande zote. Natuma ujumbe kutoka pande zote. Ujumbe wangu unakuja kupitia mikasa, vita na uvumi kuhusu vita, kupitia kwa manabii wangu na wajumbe wangu, kupitia ishara kwenye mbingu na kupitia midomo ya watoto wachanga. Hamtakuwa na sababu yo yote mkiachwa. Hamtamlaumu ye yote ila ninyi wenyewe mkiachwa kuyakabili yajayo.

Kitabu changu kimeonyesha wazi nyakati hizi mnazoishi kwa sasa, na yale ambayo yanawadia kutendeka. Wana, mnahitaji kuamka na kufuata huu ukweli ambao ninawaambia. Msisimame kama watu ambao sijawapa chochote cha kuwaelekeza kwa uzima wa milele. Nimewapa pia maonyo. Nimewapa kitabu changu lakini ikiwa mtakataa kukifuata na kuyapuuza maneno yangu na maonyo ninayowapa, sitaweza kuwasaidia. Nimekuwa wazi sana na ujumbe wangu ninaowapa. Hamtakuwa na udhuru yoyote mtakaposimama mbele yangu ikiwa mtakataa kufuata niwaambiayo. Ninaweza kuwaomba ili myatilie maanani lakini mkikataa kunisikiza sitawalazimisha. Ni kwa hiari yenu kuamua. Uamuzi ni wenu.

2 Petero 3:3-4. Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao  tamaa zao wenyewe na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali hiyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa.

Ni wachache sana watakaofanya uamuzi wa kweli au hata kufanya uamuzi wowote. Kutofanya uamuzi ni sawa na kumchagua adui wangu. La kuhuzunisha ni kuwa kuna wale ambao hawatafanya uamuzi wowote na wataendelea kuwa katika mamlaka na nguvu za adui wangu. Jambo hili linanihuzunisha mno kwa maana nililipa gharama kuu kwenye kilima cha Kalivari, ili wanangu wapate kuwa huru, huru kutoka kwa mitego

1 ... 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17
Go to page:

Free e-book «Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗» - read online now

Comments (0)

There are no comments yet. You can be the first!
Add a comment