readenglishbook.com » Religion » Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗

Book online «Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗». Author Susan Davis



1 ... 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17
Go to page:
katika Kristo Yesu wataudhiwa.

Sitadhihakiwa. Dunia haiwezi kuendelea jinsi ilivyo ikiamini kuwa hakutakuwa na matokeo. Nimechoka kukinga na kujali juu ya dunia ambayo inanidhihaki na kunichukia. Enzi hii i karibu kwisha. Hivi karibuni nitaiacha dunia ifanye itakavyo. Itakuwa dunia bila Mungu wao ambaye anaweza kuzuia maovu ambayo yatendeka kutotendeka. Dunia hainidhamini mimi kama Mungu wake. Kwa hivyo nitaiacha ili ipate kile ambacho inatamani. Ijiendeshe bila mimi Mungu Mtakatifu. Dira yake. Ndipo dunia itagundua umuhimu wa kuzishika njia zangu, sheria zangu, na kuzifuata njia zangu za milele. Wanangu watakaoachwa watashuhudia dunia isiyo na kizuizi. Utakuwa wakati mbaya kwa wanadamu. Msiachwe nyuma. Njooni kwangu. Msingojee. Jiosheni kwa damu yangu na kwa neno langu. Lisomeni neno langu. Tubuni na kuyatoa maisha yenu kwangu. Niacheni niwaokoe kutoka kwa yajayo. Ninataka. Muda ni mfupi. Fanyeni hima. Hii ndiyo saa ya kukimbilia mikononi mwangu. Upendo wangu wawangojea. Niacheni niwaokoe kutokana na maovu yajayo. Njooni niwafunike na damu yangu ili muwe salama. Nina haja ya kuwaokoa. Maneno haya ni ya kweli na halisi. Huyu ni BWANA wenu, YAHUSHUA, MKUU WA KUOKOA.

 

SURA YA 35: HAKUNA MANUFAA YOYOTE KUIKIMBIZA DUNIA INAYOKUFA

Natuanze tena. Wana, huyu ni BWANA wenu anayezungumza nanyi. Wanangu, naja hivi karibuni kwa hivyo msifadhaishwe. Dunia hii haina wakati wa kuyarekebisha mambo. Hivi karibuni, watakaokataa kurekebisha mambo kupitia kwa njia ya kutubu na kujitolea kwangu kikamilifu watateseka. Adui wangu ana kiu ya damu na hana huruma. Dunia itaona uovu ambao haijawahi kuona tangu awali. Wakati huu unakaribia kwa upesi. Sistahamili tena dunia hii mbovu na sugu. Nimesikia na kuona ya kutosha. Ni dunia inayomkataa Mungu wake na kuzipa kisogo njia zake na ukweli wake.

Yakubu 4:4. Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu?

Wana, mnaongozwa na vipofu ikiwa mtaendelea kukimbia ovyo ovyo mkitafuta mambo ya dunia. Hakuna manufaa yo yote kwa kuikimbiza dunia ambayo yafa. Haina mwelekeo wa kiadili. Ni sharti muwe mnayaona haya sasa. Ukubalini ukweli. Hakuna matumaini kwa dunia hii ambayo yafa kwa kumkataa Muumba wake. Kuweni macho. Yafungueni macho yenu. Mnaongozwa mbali na njia yangu nyembamba. Wana, ni wachache sana wanaoipitia njia hii nyembamba. Amkeni! Safisheni macho yenu na kuyatoa magamba ambayo yanawafanya msione. Njooni kwangu niwape macho ya kiroho. Niacheni niwaonyeshe ukweli. Acheni kucheza na adui mkidhani ni mchezo mwema. Ni muuaji. Atawashambulia wakati ambao hamtarajii. Hamwezi kumshinda bila mimi. Ni lazima mnisongelee ili niwakinge. Mtakuwa salama tu mnaponisongelea. Mtanusurika tu ikiwa mtakisoma kitabu changu na kuwa na uhusiano nami. Je, mnayaelewa haya? Msijidanganye. Msiwe wapumbavu. Moyo wa mwanadamu ni mdanganyifu. Adui wangu ni mjanja sana. Ninyi hamwezi kukabiliana na ujanja wake. Ni uhusiano kati yangu nanyi ndio unaoweza kuwapa ushindi ikiwa mu karibu nami, karibu sana, adui hatawakaribia kwa maana giza haliwezi kustahamili nuru. Kwa hivyo, nipeni maisha yenu na mipango yenu. Nipeni ili niyageuze majivu kuwa uzuri. Niacheni niwaonyeshe mapenzi yangu kwa maisha yenu. Ninaweza kuwatendea. Ni tayari kuwatendea. Ni hamu yangu ninyi muwe kwa mapenzi yangu. Hamu yangu ni kuwaosha kwa damu yangu na kuwaleta karibu nami jinsi mama ampendavyo mwanawe, hivyo ndivyo natamani kuwashughulikia.

Isaya 66:13. Mfano wa mtu ambaye mama yake amfariji, ndivyo nitakavyowafariji ninyi; nanyi mtafarijiwa katika Yerusalemu.

Mathayo Mtakatifu 23:37. Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!

Wana, saa hii ya kurudi kwangu inakaribia. Hamtazami. Mtaachwa. Nawajia tu wanangu ambao wanatazamia kurudi kwangu, wanaotamani kunitafuta kwa uhusiano wa ndani. Hawa ndio wajao nami. Wengine wote, watabaki. Wengi kati yao watapotea kwa maangamizi ya ghafula. Huu ni wakati wa kutilia maanani maonyo haya. Someni kitabu changu. Zifungueni kurasa zake. Ombeni Roho wangu Mtakatifu awaongoze katika ukweli. Wakati unaisha. Msipoteze hata dakika moja mkikimbiza dunia ambayo inanichukia, Mungu wenu. Mnaelekea kwa upande wa mauti. Jirudini. Nitafuteni. Mtafuteni Roho wangu; mtafuteni baba yangu, tutafuteni. Sisi ni kitu kimoja na sote tunataka kuwaokoa. Wakati wa kurudi kwangu umewadia. Msikose wokovu wangu. Huyu ni BWANA WENU YAHUSHUA, awapendaye kwa dhati.  

 

SURA YA 36: WENGI WADHANIAO KUWA WA TAYARI WAJIDANGANYA

Natuanze binti yangu (Machi 4, 2012). Sikiza kwa makini ninapokupa maneno haya mwanagu, huyu ni BWANA. Tafadhali yaandike maneno haya: wakati wa kurudi kwangu unakaribia. Wengi wangali hawatazamii. Wengi wana pazia za macho na wanakataa kusikiliza niwaambiayo. Saa ya kurudi kwangu yaja haraka. Ni sharti mjitayarishe wanangu. Ni sharti mjiandae. Kuweni macho mkitazama. Ni muhimu kufanya maandalizi. Wale wanaotazamia ndio tu watakaochukuliwa. Wale walio na haja ya kujua kurudi kwangu ndio watakaochukuliwa pekee yao. Wale wasiojali na wasio kaa kwenye roho wangu watabaki na kukabiliana na uovu. Wengi watashangaa kuwa wameachwa. Wengi watashtuka kuona kuwa wameachwa. Wengi wanaofikiria kuwa wa tayari watashangaa kuona wameachwa. Wengi wadhaniao kuwa wa tayari wajidanganya. Hawako tayari hata kidogo. Wamefungwa na vitu vya dunia. Fikira zao zi kwenye mambo ya dunia. Hawajali kutazamia kurudi kwangu. Wanajishughulisha na mambo ya dunia. Hawana wakati nami. Hawanitazamii.

Wanakejeli na kuwatesa wanitazamiao. Watashikwa na bumbwazi watakapoachwa nyuma wakidhani kuwa wananijua. Hawanijui hata kidogo. Wanadhani tu wananijua. Mioyo yao i mbali nami. Hawaji kwangu mahali pa siri. Wanayakimbilia mambo ya dunia. Macho yao hayanitazamii. Wanapenda kushika na kushiriki na mambo ya dunia. Wanapangia mambo yajao. Wanafanya mipango ambayo haitatendeka. Hawaniulizi kuhusu mipango hii. Wangeniuliza ningewaambia wanitazame mimi, waje karibu nami, na kuniachia mipango yao. Hili ndilo ninalohitaji. Mjitolee kwangu kikamilifu. Iwekeni mipango yenu miguuni pangu. Nipeni maisha yenu na mipango yenu ya siku zijazo. Mimi tu ndiye ninayeelewa mambo yajayo. Mipango yote mliyonayo yaweza kuvunjika wakati wowote. Mbona msiniache niwapangie mipango yangu niliyonayo kuhusu maisha yenu? Najua yaliyomema kwenu. Najua mwanzo na mwisho. Mimi ni ALFA na OMEGA. 

Ufunuo wa Yohana 22:13. Mimi ni ALFA na OMEGA, Mwanzo na Mwisho, wa Kwanza na wa Mwisho.

Mimi ni muumba wa jua, mwezi, na nyota. Mnadhani siwezi kujali kuhusu maisha yenu ya baadaye? Ninaweza kuwaleta ufalmeni mwangu ikiwa mtanipa maisha yenu. Nitawapa amani na usalama, nitawabeba hadi mahali pa usalama. Mtaishi kwa amani mkijua kuwa mipango yangu kwenu ni miema na nitaitimiza. Mtakuwa na usalama huu ikiwa mtakaa ndani ya mapenzi yangu, maishani mwenu. Hamtakuwa na wasiwasi tena mkiwa ndani ya mapenzi yangu. Achilieni mipango yenu na maisha yenu. Itawaongoza tu kwa uteketezi. Nitoleeni kila kitu na mwingie kwa mapenzi yangu. Mapenzi yangu kamili. Muachieni ajuaye mwanzo na mwisho ayaongoze maisha yenu. Mimi ni MUNGU wenu aishiye milele. Nitawaleta kwa ufalme wangu wa milele. Ni wenu mkiuliza.

Ufunuo wa Yohana 21:6. Ananiambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, chemichemi ya maji ya uzima bure.

Jitoleeni, tubuni, na mnifanye kuwa wenu. Mnijue. Nitaufungua moyo wangu kwenu. Natamani kutembea nanyi. Hamtakuwa pekee yenu. Kwa hivyo, wakati wa kunipa yote ni sasa. Hii ndiyo saa. Chagueni kwa hekima. Kuna nia nyingi. Njia moja tu ndiyo ya kweli, njia moja tu ndiyo nyoofu. Mnijue na nitawaongoza kwa njia nyoofu. Hii ni tamaa yangu. Kuwaongoza.

Waebrania 12:13. Mkaifanyie miguu yenu njia za kunyooka, ili kitu kilicho kiwete kisipotoshwe, bali afadhali kiponywe.

Hivi karibuni saa itagonga saa sita za usiku. Ikimbilieni mikono yangu. Mikono salama. Niacheni niwaokoe. Chagueni haraka. Yanihuzunisha kumwacha ye yote ila chaguo ni lenu. Msisite kuupokea upendo wangu.

YAHUSHUA, MUNGU wa upendo mkuu.

1 Yohana 4:16. Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

 

SURA YA 37: MNA WAKATI MDOGO SANA ULIOBAKI

Natuanze. Nitakupa maneno mengine: Wana, ni mimi BWANA wenu na nina maneno ya kuwapa.

Saa inachelewa. Nuru iliyobaki kwa siku ni ndogo sana. Ni sharti mjitayarishe. Jitayarisheni kwa maana wakati wa kurudi kwangu u karibu sana. Unatimia. Ni wachache sana walio tayari na wangojao. Ni wachache sana wanaojali kujitayarisha. Wengi wamechagua kutosikiza maonyo yangu. Wengi hawajali kuhusu yajao. Saa inakaribia. Nawataka muwe macho na kuwa tayari. Msipofanya hivyo, mtapatwa bila kujihadhari. Ikiwa hamtazami, hamtayaona yajayo. Wale wanaotazamia ndio watakao kuwa macho. Hao pekee ndio watakaokuwa wamejiandaa. Utajiandaa kivipi ikiwa hautazamii? Wale tu ambao wamejiandaa na kujitayarisha ndio watakaoenda pekee yao. Wengine wote watakuja na taa zisizo jaa mafuta.

Mathayo Mtakatifu 25:7-10. Mara wakaondoka wanawali wale wote wakitengeneza taa zao. Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika. Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, sivyo; hayatutoshi sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie. Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.

Huu si wakati wa kusinzia wanangu. Hii siyo saa ya kulala. Siji kuwachukua wale ambao hawawezi hata kukesha wakinitazamia. Wale walalao wataamka na kukumbana na tisho wasiloweza kulikabili. Ni wakati wa huzuni sana kwa kanisa langu linalo lala.

Waebrania 9:28. Kadhalika Kristo naye, akishakutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi, atatokea mara ya pili pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu.  

Wanangu wamelala fofofo na wasipoamua haraka, watajipata kwa mikono ya adui wangu. Hana huruma na yeyote. Ni fedhuli. Ana kitu kimoja tu akilini mwake: Nguvu na mamlaka ya kuongoza. Atatawala kwa nguvu. Siwezi nikawafanya muelewe kwa undani atakayofanya. Huu ni wakati mgumu sana na kuna mambo mazito yajayo duniani. Sifurahii kuwaelezea mambo haya. Ninawaonya tu kuhusu yajayo kwa sababu sitaki mteseke kwa mikono ya adui wangu kwa ajili ya yale ambayo hivi karibuni yataikumba dunia. Jirudini wanangu. Amkeni kutoka usingizini. Ondoeni pazia machoni penu. Njooni kwangu haraka. Wakati uliobaki ni kidogo sana. Nikimbilieni kwa upesi. Nataka niwaokoe kutoka kwa maafa yajayo. Msipatwe na dhoruba inayokuja. Ni wachache sana watakaokuja nami nirudipo kumchukua bi arusi wangu. Ni wachache sana ambao wamechagua kunitazamia na kujiandaa kupitia kuoshwa na neno na damu yangu. Hakuna majibu. Hakuna njia nyingine.

Waefeso 5:25-27. Enyi waume wapendeni wake zenu, kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa kwa ajili yake; ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; apate kujiletea kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lolote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.

Jitoleeni kwangu sasa. Ni tayari

1 ... 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17
Go to page:

Free e-book «Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗» - read online now

Comments (0)

There are no comments yet. You can be the first!
Add a comment