readenglishbook.com » Religion » Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗

Book online «Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗». Author Susan Davis



1 ... 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17
Go to page:
kutawaokoa. Hakuna njia nyingine. Mkigeukia dunia kuwapa majibu, mtapotoshwa na uongozi wa watu wasionijua wala kuujua ukweli wangu. Hii saa inakaribia. Jitengeni na dunia. Isafisheni mikono yenu kuondoa uchafu dunia inayowapa. Dunia inawatoa kwangu. Njooni karibu nami. Nitazameni mimi. Mimi ndiye mwokozi wa mwisho kabla dunia kuisha. Msikose wokovu huu ambao ndio wa kipekee na utakao wapeleka kwa usalama.

 Waraka wa Yakobo 4:8. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.

Jitayarisheni kuwa mmoja wa bi arusi wangu. Njooni kwangu kwa kujitolea kikamilifu. Maisha yenu yote yatoeni kwangu. Nipeni kila kitu chenu na utii wenu. Nitawaongoza kwa usalama. Hii ndiyo ahadi yangu kwenu: usalama na uhuru kutokana na yale yatakayo kuja duniani hivi karibuni. Msikatae. Msiishi ili kujuta uamuzi wenu siku moja. Mimi hulitimiza neno langu. Naweza kuwapeleka kwenye usalama. Mimi ni MUNGU mwenye nguvu. Ni mwaminifu. Msifadhaike mioyoni mwenu. Ikimbilieni mikono yangu ya wokovu.

MUNGU wenu mwaminifu, YAHUSHUA.

 

SURA YA 32: NI KARIBU KUMUONDOA BI ARUSI NA KUMPELEKA MAHALI PA USALAMA

Binti yangu, hebu tuanze (Februari 28, 2012). Wana, mimi ni MUNGU wenu. Mimi ni MUNGU anayewajali sana. Nawatakia tu mema. Sasa wanangu, nataka myasikie maneno yangu. Nisikizeni kwa makini. Dunia i karibu kuangamia. Hivi karibuni dunia itageuka. Ni mengi sana yatatendeka ndani na pande zote na ni machache tu yatakayokuwa mema. Nauondoa mkono wangu wa kinga kutoka duniani, kwa maana dunia imeniasi. Inatembea kinyume na moyo wangu, njia zangu, ukweli wangu. Ni makuruhi kwangu. Ni karibu kuwaruhusu mbwa na shetani, kurithi dunia.

Zaburi 22:16. Kwa maana mbwa wamenizunguka, kusanyiko la waovu wamenisonga; wanizua mikono na miguu.

Tukio li karibu. Wanangu, siku zijazo zitakuwa siku za giza. Sistahamili uovu tena duniani. Ni karibu kumuondoa bi arusi wangu na kumpeleka mahali pa usalama. Hivi karibuni nitamuondoa. Sitavumilia yanayotendeka duniani tena. Ni karibu kuitema dunia. Uovu ambao umetanda duniani ni uvundo usoni mwangu. Siwezi kuutazama. Sitawaruhusu wapendwa wangu waendelee kustahamili dunia. Kanisa langu li karibu kuondolewa ili lipelekwe kwa usalama. Saa hii inakaribia kwa upesi sana. Enyi wana, mbona mna tashwishi? Muamini musiamini, tukio hili litatendeka. Ni lazima litendeke kama ilivyo kwenye kitabu changu. Nimewambia ukweli. Nimewaeleza kuhusu siku za mwisho kitabuni mwangu. Yasomeni maneno yangu. Jizoezeni na kitabu changu. Myasome maneno kwa makini. Mtaona kuwa hizi ni siku za mwisho na kurudi kwangu ku karibu. Enyi wana, acheni kujadiliana. Njooni mnitafute. Njooni kwangu na mioyo mikunjufu nami nitawaonyesha ukweli. Natamani kuwafichulia ukweli. Mimi siwapotoshi wanangu. Wakiamua kutonifuata basi siwezi kuwafichulia ukweli. Wataendelea kwenda kwenye uchochoro usotoka, na njia za kuangamiza. Njooni nami ili mpate njia. Nitawaongoza kwa njia yangu nyembamba. Ni wachache wanaoipata. Wanangu, wachache wanaitafuta njia hii. Msiwe miongoni mwa wale wengi wasioipata njia hii. Kuna wengi sana ambao wamepotea njia. Wengi sana walio kwa njia pana ambayo itawaangamiza.

Mathayo Mtakatifu 7:13. Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.

Jirudini wanangu. Changamkeni. Nitafuteni kwa bidii. Hakuna njia zingine ziendazo kwa uhuru na uzima wa milele. Saa ni hii. Kimbilieni mikononi mwangu. Msisite. Kusita kutasababisha mwisho wenu. Nataka kuwaokoa. Jitoleeni kwangu kwa kila njia. Nipeeni maisha yenu yote. Kutojitolea kikamilifu hakutoshi. Njooni kwangu na kuyatoa maisha yenu. Nitayapokea na kuwatukuza kwa ajili ya mipango yangu ya ninyi kunitumikia kisha mje kufurahia mbinguni milele.

Yeremia 30:19. Tena kwao itasikiwa shukrani, na sauti yao wachangamkao; nami nitawazidisha, wala hawatakuwa wachache; tena nitawatukuza, wala hawatakuwa wanyonge.

Saa hii inakwisha. Adui wangu ameanza kujitokeza. Hivi karibuni nyote mtajua kuwa mnaishi kwa wakati gani; ila huenda ikawa mumechelewa sana kuokolewa na mtakuwa mumepoteza nafasi ya kuokolewa. Wanangu, najaribu kuwaamsha na kuwaletea ukweli. Nitafanya nini ili mnisikize? Mkingoja sana kunijia mtaachwa nyuma. Itanibidi niwaache nyuma. Msiache jambo hili litendeke. Kutubu, kujitolea na kunisongea: Haya matatu ndiyo ninayotamani kwenu. Haya ndiyo mnayohitaji ili muingie katika ufalme wangu. Kitabu changu si kinanena hivi? Njooni upesi bila kuchelewa. Njooni na nitawasafisha na damu yangu na mtakuwa tayari kusimama mbele yangu na kupokelewa ufalmeni mwangu, ufalme wangu wa milele.

Ufunuo wa Yohana 1:5. Tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake.

Wakati unakwisha. Msipoteze hata dakika nyingine moja duniani humu. Huyu ni BWANA na MFALME wenu anayenena nanyi. Aliye juu na mwenye nguvu, aliye na mamlaka ya milele BWANA YAHUSHUA.

 

SURA YA 33: AIDHA MNIPE NAFASI YA KWANZA AU MSINIPE NAFASI YO YOTE ILE

Hebu tuanze (Machi 1, 2012). Wana, huyu ni Bwana wenu. Nina maneno mapya ambayo nataka kuwaelezea: Wanangu, kuna kipindi kipya ambacho kinataka kuanza duniani. Kipindi cha uovu. Watu waovu, nyakati mbovu. Ni sharti mjitayarishe kuondoka nami. Nawataka muwe tayari. Nitahitajika kumkuta bi arusi nimuondoe katika dunia hii mbovu na kumpeleka kwa usalama. Siwezi kumueka hapa duniani tena, kwa sababu hivi karibuni dunia hii itakuwa mbovu na isiyopendeza. Bi arusi ni sharti afichwe kwa usalama. Kisha dunia itaanza uovu wake kwa watakaobaki. Hivi karibuni, tukio hili litatendeka. Hata sasa tufani zote zajaa ili kuanzisha tufani kuu ya uharibifu, uoga mkuu ambao utawashinda wanadamu ambao watachagua kwenda kinyume nami. Ni sharti nipewe nafasi ya kwanza maishani mwenu ili mzuie tisho hili lijalo.

Mimi si Mungu anayetamani kuwaona wanawe wakiteseka, ila mkikataa kuniweka juu ya miungu mnayoiweka mioyoni mwenu, basi hivi karibuni mtajifunza maana ya kumkataa MUNGU wenu, MUUMBA wenu. Mimi si Mungu wa kufanyiwa mzaha. Nataka nipewe nafasi ya kwanza au nisipewe nafasi yo yote ile. Sitaki kupewa nafasi ya pili au ya tatu kwa orodha zenu. Niliwaumba kwa manufaa yangu. Mniabudu, mnitukuze na kunijua. Natamani kuwa na uhusiano wa karibu sana nanyi. Mkiamua kutonijua kwa njia hii, basi mtapata njia zenu na tutaachania hapa. Nendeni mhusiane na adui wangu mahali pake pa milele. Mimi ni MUNGU aliye na wivu. Sikuwaumba ili nishiriki nanyi na adui wangu.

Kumbukumbu La Torati 32:16. Wakamtia wivu kwa miungu migeni. Wakamkasirisha kwa machukizo.

Aidha mnataka kuwa wangu tu au mwaweza kuifuata ile njia pana itakayo wapeleka upotevuni ambako wengine tayari wameshaenda huko. Ni wachache sana wanaotaka kunijua kuliko kufuata mambo ya dunia. Je, ni wapi maishani mwenu? Sistahili kupewa nafasi ya kwanza maishani mwenu? Niliwafia wanangu kifo kiovu cha uchungu mwingi! Niliwaumba na nikawapa uhai. Nawahimili kila siku. Wanangu, hivi karibuni itabidi muamue. Mnataka amani, utulivu, na upendo wangu? Mnataka hakikisho langu la kuwapeleka kwa usalama kutoka kwa dunia ambayo inakwisha? Basi hii ndio saa ambayo mtaamua mtakalofanya. Mtamkubali vipi Mungu wenu? Kwa upendo na utiifu au kwa uvuguvugu?

Wafilipi 2:8. Tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

Nawataka muamue. Mtajitolea kufa kwa ajili ya miili yenu na kunitolea yote? Nawangojea mje kwangu, mtubu ili niwafunike kwa damu yangu. Ni kwa kupitia damu yangu tu ndipo mtaokoka. Kwa dhabihu niliyotoa msalabani. Mkikubali zawadi hii ya gharama ya damu yangu, mtubu dhambi zenu kwa mioyo mikunjufu, myatoe maisha yenu kwangu na kunifuata bila kusita, nitayabadilisha maisha yenu, niwasafishe na kuwaandaa kuingia kwa ufalme wangu. Niwaweke kuwa tayari kuja nami. Zingatieni sana haya. Wana, msingojee sana. Kungojea ili kuona litakalotokea na kutoamua haraka kwaweza kusababisha kutoona niliyowaandalia kwa uzima ujao. Msiwe wajinga. Jirudini. Kuweni tayari. Nataka muokoke kutoka kwa tisho lijalo. Nawaombeeni. Nawaombeeni kwa baba yangu kwa ajili yenu. Wana, wakati huu unadidimia. Nawataka mfanya uamuzi. NITAMJIA BI ARUSI WANGU! Msikose kushiriki. Msikose yote niliyowaandalia. Sidanganyi. Nitashinda na kanisa langu pia litashinda! Kwa hivyo, ni sharti myatilie maanani ninayowambia. Ni mimi NIKO ambaye NIKO. NI BWANA YAHUSHUA ambaye ni mwaminifu kwa ukombozi.

 

SURA YA 34: KUNA DHIKI YAJA—DHIKI KUU.

 Natuanze (Machi 2, 2012). Wanangu, ni mimi BWANA wenu. Nina maneno mapya ya kuwapa. Wana, huu ni wakati wa kutilia maanani. Kuna simanzi kuu yaja duniani. Kutakuwa na hatari kubwa na huzuni. Shida hizi tayari zimeanza. Dhambi imeenea miongoni mwa wanadamu wote. Msifadhaike, nimeshinda dunia. Naja kumuondoa bi arusi nimpeleke mahali pa usalama. Ni mrembo na mzuri ajabu. Anatazamia kurudi kwangu. Kurudi kwangu hivi karibuni. Ananitazama mimi pekee. Nampenda kwa moyo wangu wote. Namkumbatia kwa macho yangu. Namtazama po pote aendapo. Hatoki machoni pangu. Hivi karibuni atakuwa nami mbinguni kwa usalama huku dunia atakayoiacha ikiwa inapasuka.

Yohana 16:33. Hayo nimewambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwengu unayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.

Tukio hili limeanza kujitokeza wanangu. Kuna dhiki yaja – dhiki kuu. Dunia haijawahi kuona tukio kama hili. Ninyi nyote hamtilii maanani maonyo yangu, ishara zangu, kitabu changu. Je mnaelewa kuwa mashaka yaja duniani? Yaja na hakuna binadamu yeyote awezaye kukomesha. Chanzo ni ulimwengu huu ambao umemkataa MUNGU wake. Dunia haijali kunihusu au kuhusu njia zangu. Kwa hivyo ni sharti niuondoe mkono wangu wa kinga na kumuondoa bi arusi wangu. Hivi karibuni, dunia itaelewa maana ya hofu kuu.

1 Yohana 4:1-8. Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. Katika hili mwamjua Roho Wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mugu. Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya Mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani. Ninyi watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni Mkuu kuliko yeye aliye katika dunia. Hao ni wa dunia; kwa hivyo wanena ya dunia na dunia huwasikia. Sisi twatokana na Mungu. Yeye amjuaye Mungu atusikia, yeye asiyetokana na Mungu hatusikii. Katika hili twamjua Roho wa kweli, na roho ya upotevu. Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye amjua Mungu. Yeye asiyependa hakumjua Mungu, kwa maana Mungi ni upendo.

Sitawadanganya enyi wana. Mimi ni MUNGU. Dunia hii haitakuwa mahali ambapo mtatamani kubakia kuona yatayotokea baada ya tukio hilo. Hamtaweza kustahamili yajayo ikiwa mnataka kuwa ndani yangu. Wote watakao nikiri baada ya bi arusi wangu kuondolewa watakufa kwa ajili ya imani yao. Utakuwa wakati mgumu kwa wanangu. Msiwe wapumbavu kufikiria visivyo.

2 Timotheo 3:12. Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa

1 ... 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17
Go to page:

Free e-book «Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗» - read online now

Comments (0)

There are no comments yet. You can be the first!
Add a comment