readenglishbook.com » Religion » Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗

Book online «Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗». Author Susan Davis



1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 ... 17
Go to page:
mapenzi yangu, na nikama kipofu akimwongoza kipofu kwa vichochorofunge vya uteketezi. Wengi watastaajabu jinsi walivyodanganywa kwa sababu waliwategemea watu wasionijua na wakadanganyika sana.

Huwezi kuweka imani yako kwa mambo ya dunia yanayoonekana kana kwamba ni ya ukweli. Lazima unitii.  

Niachie yote na unitafute kwa moyo wote. Hili ndilo jambo ninalohitaji.

Neno langu linanena juu ya ukweli huu. Lisome vyema na ujionee. Viongozi wangu wengi wanaupenda ulimwengu na mambo yake, kwa hivyo hao hulibadili neno langu ili wajihisi vyema wanapo changanyika na dunia. Dunia ni adui wangu. Lisome neno langu. Ukweli huu haujafichika. Huwezi kunipenda na pia upende dunia. Hatutangamani. Nimewaeleza kinaganaga kuhusu haya. Ni kweli, umo kwenye dunia lakini lazima unifuate na uzifuate njia zangu wakati ungalipo duniani.

Yakubu 4:4. Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.

Kuna vivuta mawazo kila uendapo ambavyo vinawaongoza watu na kuwafanya wasiwe na uhusiano wa ndani nami. Ni lazima muwe na tamaa ya kutaka kukaa nami kuliko vivuta mawazo vya dunia. Utakuwa unakubali kitu duni ikiwa utakimbilia mambo ya dunia kuliko kuwa na uhusiano na Muumba wa uhai wote – Muumba wako, Muumba wa nyota na mbingu.

Waebrania 10:38-39. Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; naye akisitasita, roho yangu haina furaha naye. Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa roho zetu.

Usibadilishane utukufu wa milele nami Muumba na Mwenye kupa riziki kwa uhai mwingine wo wote na raha duni upewazo na dunia. Unavyovifuata duniani ni vitu visivyo na maana ambavyo hatima yavyo ni kifo. Mnachagua hatima zenu, mnaziamini njia zenu, na kuamini kuwa ninabariki uamuzi wenu. Hamjanijua kwa karibu na undani. Mngalifanya hivyo, mngalijifunza tofauti. Mnadanganywa na njia za dunia na huyo adui wangu mjanja. Anawafanya mtende mambo mnayoamini ni mema bila mimi. Siwezi kubariki njia kama hizi. Kisha mnashangaa kwa nini mnapatwa na mateso mengi. Undanganyifu mkuu kutoka kwa adui wangu ni kule kuamini kuwa mambo yote ni shwari wakati unafuata ulimwengu bila uhusiano wa karibu na mimi. Huu ni udanganyifu mkuu kushinda zote. Yote yanaonekana sawa lakini wakati wa hukumu nitawaambia; siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

Mathayo Mtakatifu 7:21. Si kila mtu aniambiaye Bwana, Bwana atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye Mbinguni. Wengi wataniambia siku ile Bwana, Bwana, hatakufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Ndiyo, hili ni neno langu. Sikuwaumba ili mwende mbali nami na kujitafuatia njia zenu wenyewe bila kunishauri. Ndiyo, mnaweza kutenda haya yote maanake mna hiari, ila hamko kwenye hiari yangu na kwa hivyo mnatenda dhambi dhiidi yangu.

Nawapa wanangu hiari na wanaweza kuchagua kunitafuta kwa ndani na kuamini uongozi wangu au waweza kwenda mbali nami. Wanangu wanapoenda mbali name, nje ya mapenzi yangu, wakitafuta mipango yao wenyewe, wanatenda kazi dhidi ya mipango ya ufalme wangu, na huu ni uovu. Wana sababisha uharibifu wasiojua hata kidogo, kwa sababu wamejiamini kuwa wanaweza kuishi maisha yao nje ya mapenzi yangu mema na mipango yangu. Wanajiletea shida na kuwaletea wengine pia. Wanajiweka wazi kwa mitego na mipango ya adui. Wanangu, bila mimi, hamuwezi kushindana na ujanja na hila za adui wangu. Msijifikirie wenye busara sana. Ninyi ni bure bila mimi.

Mbona ninasema kuwa walio na imani kama ya mtoto ndio watakaourithi ufalme wangu? Ni kwa sababu wanatambua kuwa wananihitaji wakati wote jinsi mtoto anavyo mtazamia mzazi wakati wote. Mtoto anajua bila mzazi yumo hatarini. Hivyo ndivyo wanaangu wana tambua kuwa bila mimi watakuwa kwenye hatari kuu na kuamini kila neno ninenalo. Hii ndiyo maana nawasihi wanaangu wawe na muda kwa neno langu ambalo litawaelimisha.

Majibu kuhusu jinsi ya kuishi maisha haya yamo kitabuni mwangu. Niliwapa kitabu hiki kama kielekezi kwa wanadamu.

Roho wangu anaufichua ukweli katika kurasa hizi. Ni kwa kupitia kutii na kumpokea Roho wangu kwa kipimo kikamilifu ndipo utapokea utaalamu unaohitaji ili kuyaelewa maneno yangu kikweli. Sio kuwa kupitia mafunzo ya binadamu, bali kwa Roho wangu ndio maneno yanakua katika moyo wako. Ni kwa kupitia kwa Roho wangu tu ndipo utapokea uzima wenye nuru upatikanao kwenye kitabu changu.

Mathayo Mtakatifu 18:4. Basi yeyote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.

1 Wakorintho 2:11-14. Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajwa tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu, maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.

Ulimwengu wa sasa umejaa udanganyifu. Msidanganywe na uovu unaokuzwa na adui wangu. Anataka muamini kupitia ujumbe mnaoupata kila siku kwamba mnaweza kuviamini vitu vya dunia. Mnaweka imani yenu kwa vitu vingine vyote isipokuwa Mimi, niwapaye uhai. Mnaweka imani yenu kwa pesa, elimu, usalama wa dunia, serikali. Huu ni msaada wa uongo. Huu ni udanganyifu wa hali ya juu na unawapeleka wanangu mbali nami. Wanangu wanaanza kuniamini kijuujuu. Wanakuja kwangu kidogo kisha wanategemea vitu vingine kuliko kunitegemea mimi. Huu sio uhusiano wa ndani.

Ndiyo, mna uhusiano wa ndani na dunia na matamanio yenu wenyewe. Lakini hamna uhusiano wa ndani nami. Mnatakiwa mnirudie na kuweka kila kitu mbele yangu. Hamuwezi kunijua kikweli hadi mtakapoweka kando usalama wa kidunia na kuja kwangu mkifuta uhusiano wa ndani. Chochote kile mbali na uhusiano wa aina hii ni uhusiano vuguvugu nami sitaheshimu uhusiano vuguvugu. Wengi watashangaa watakapokuja mbele yangu na kugundua kuwa kucheza dansi na dunia na kuwa na wakati mchache nami utawaweka nje ya ufalme wangu. Kutakuwa na wengi sana watakaoshikwa na mshangao.

Ufunuo wa Yohana 3:16. Basi, kwa sababu una uvuguvugu wala hu baridi wala si moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

Ni nini ninachotaka na kutarajia kutoka kwa wanangu? Nataka maisha yao. Nayataka yote kwa utiifu kamili. Ku dansi nami kisha unaenda na kudansi na ulimwengu ni uovu. Lisomeni neno langu. O! Wengi hulisoma neno langu na kuchukua maneno watakayo ili wajitulize ndio waendelee na raha za dunia huku wakijiona kuwa wataingia katika ufalme wangu maisha yao yaishapo. Utakuwa mshtuko ulioje kwa wale watakaogundua kuwa nawapokea wale tu waliojitolea kikamilifu kwa yote – waliojitolea mhanga. Ole wao watakapogundwa kuwa kumbe kule kufuata mali na umaarufu, ilikuwa kazi bure na iliwaweka nje ya ufalme wangu. Hiari yao na mipango yao ya siku zijazo iliwaongoza kwa njia iliyo mbali na mapenzi yangu na mipango yangu kamili kwa maisha yao – maisha niliyo wapa.

Ndio. Hakuna yeyote apumuaye siku kwa siku bila idhini yangu. Hii ndio maana wanangu wasiwe na uhakika sana juu ya mipango yao ya kibanafsi iliyo mbali na mapenzi yangu, na makusdio yangu ya kweli kwa maisha yao. Naweza kuuchukue uhai wo wote ule nitakao kwa hiari yangu. Hakuna aishiye kando na maamuzi yangu kwa maisha yao. Nawapa, nachukua kulingana na vile nionavyo bora. Ndio maana ni ujinga wakati wanadamu wanajiundia mipango yao nje ya mapenzi yangu kwa maisha yao. Ni kiburi na ujinga na ni uovu. Hii ndiyo njia adui wangu anayoitumia kuwaongoza kondoo wangu kwa njia potovu akitumia mambo yanayoonekana sawa na kawaida. Ni mpango wa adui wa kuwadanganya wengi.

Kitabu Cha Ayub 12:10. Ambaye nafsi ya kila kilicho hai i mkononi mwake, na pumzi zao wanadamu wote.

Zaburi 104:29. Wewe wauficha uso wako, wao wanafadhaika; waiondoa pumzi yao, wanakufa, na kuyarudia mavumbi yao. 

 

SURA YA 3: KUJIFUNZA UNYENYEKEVU

Binti, ni tayari kukupa maneno. Usikilize kwa makini ninapozungumza. Nataka kukupa taarifa mpya. Nataka kuzungumzia kuhusu kujifunza njia ya kuwa mnyenyekevu.

Hii ndiyo njia ya wanyenyekevu. Wenye moyo mpole na mtulivu ndio wanangu wanyenyekevu. Wanaenda kwa upole bila kutafuta cheo au marupurupu. Wananitafuta kwa njia zote. Kila kukicha wanamtafuta Mungu wao. Hawataki umaarufu.

Wanatamani tu kupendwa na kutunzwa nami, Mungu wao. Wananiamini nami nawatunza. Nakutana na matarajiyo yao. Nawatimizia haja zao. Nawaletea vyote wanavyohitaji maishani mwao. Mimi ni Mwamba wao.

Ni mwaminifu wakati wote kwa watumishi wangu wanyenyekevu. Nawaletea amani na utulivu kwenye dhoruba zote. Ni upande wao kila wakati; nakaa nao kila wakati, nawatumikia kila wakati. Nawapenda watumishi wangu wanyenyekevu. Hao ni harufu nzuri kwangu. Nawapenda nao wanipenda. Hatutenganishwi. Mimi ni hewa yao. Wanameremeta kama nyota. Hawatafuti njia za dunia. Nawatosheleza. Hawayumbiyumbi na mambo ya dunia. Wananitafuta ili niwatosheleze nami nawaletea vyote watamanivyo.

Hawaudhiki. Ni wachache sana wanao tembea kwenye njia hii. Niwachache sana wanaoipata njia hii. Wale waipatao, wanapata barabara ya kwenda kwa ufalme wangu wa milele.

1 Petero 5:6. Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake.

Watumishi wangu wanyenyekevu huisikiza sauti yangu. Wanasonga ninapowambia wasonge na wananitumikia wakati ninapowahitaji kwa mioyo yenye furaha: wanapenda kutumika katika ufalme wangu. Wanatosheka kumtumikia Mfalme wao nami nawaletea furaha na amani. 

Upendo wangu unabubujika juu yao. Hawakosi cho chote.

Ili uwe mnyenyekevu, huna budi kujiweka katika nafasi ya mwisho. Usiye hitaji nafasi ya kwanza.

Ni busara kuwa wa mwisho sio wa kwanza. Wajinga hutafuta nafasi ya kwanza. Watumishi wangu wanyenyekevu wana busara na wajua kinacho nipendeza mimi, Mungu wao.

Wanangu ni wale wanyenyekevu. Wale wasio fahamika duniani na wasioonekana, wamefichika mbali na wao wapendao dunia.

Hawana maana hapa duniani, lakini kwa ufalme wangu hao ndio watawalao na watamalakio. Wameinuliwa katika umiliki wangu mbinguni. Nawaheshima wanyenyekevu wangu. Wanaketi nami kwenye kiti changu cha enzi na kufurahia kuwepo kwangu. Wanyenyekevu wanaojiweka kwenye nafasi ya mwisho kwenye maisha haya, watafurahia cheo kwenye ufalme wangu. Wanainuliwa na kuwekwa kwenye utukufu kwa ajili ya kuishi maisha ya utiifu ulimwenguni. Hawa huniletea raha na niwapa amani, amani ya milele.

Marko Mtakatifu 10:31. Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.

Natembea na walio wanyenyekevu na kujitambulisha kwao. Hii ndiyo zawadi yangu kwa kujitolea mhanga kwao. Upendo wao kwangu ni harufu iliyonzuri na nitawaheshimu.

Unyenyekevu ndiyo njia ya ufalme wa Mungu. Kila aliye kwa ufalme wangu amejazwa na unyenyekevu. Kiburi hakiwezi kuinga kwenye ufalme wangu. Hakina nafasi kwenye ufalme wangu. Utiifu wa amani ndio ulio na nafasi katika ufalme wangu. Huu ndio ufalme, mwingi wa unyenyekevu na upole. Mahali ambapo kila mmoja anatosheka na upendo na uzuri unaofurika. Hakuna asiye tosheka na maisha yake mbinguni. Matumaini na amani ni tele. Ufalme wa mbinguni umefurika kwa upendo.

1 Yohana 2:16. Maana kila kilichomo duniani, yaani tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

 

SURA YA 4: KUMWAMINI MUNGU

Natuanze binti yangu (Februari 7, 2012). Mwanangu, leo tutashughulikia jambo geni: Nataka kuzungumzia juu ya kumwamini Mungu. Wanangu hawaamini, wanasema wanaamini lakini

1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 ... 17
Go to page:

Free e-book «Marriage Supper of the Lamb (Swahili version), Susan Davis [free e books to read online .txt] 📗» - read online now

Comments (0)

There are no comments yet. You can be the first!
Add a comment